Jumatatu 11 Agosti 2025 - 07:01
Kumbukumbu za Maulamaa | Swalini Swala Mwanzo wa wakati, Umaskini Wenu Utaondoshwa

Hawza/ Ayatollah Bahjat amenukuu kutoka kwa Ayatollah Sayyid Abdulhadi Shirazi kwamba baada ya kufariki baba na mlezi wa familia, jukumu la maisha lilimwangukia yeye. Katika ndoto alimwona baba yake, akamueleza kuhusu ugumu wa maisha, na baba yake akamsia kwamba watu wa nyumbani waswali swala mwanzo wa wakati ili umaskini uondoke.

Kwa mujibu wa ripoti ya  Shirika la Habari la Hawza, Ayatollah Bahjat amesimulia kumbukumbu aliyoinukuu kutoka kwa Ayatollah Sayyid Abdulhadi Shirazi kuhusu kuondoa umaskini, na tunaiwasilisha kama ifuatavyo.

Katika utoto wangu, baada ya kufariki baba yangu na Mirza mkubwa ambaye alikuwa akisimamia mambo yetu, jukumu la kulea familia liliangukia kwangu.

Nilimwona baba yangu katika ndoto.

Akaniuliza:
“Bwana Sayyid Abdulhadi! Vipi hali yako?”

Nikamjibu:
“Sio nzuri.”

Akasema: “Waambie watoto na watu wa nyumbani kwamba waswali swala mwanzo wa wakati, umaskini wenu utaondoshwa.”

Chanzo: Kituo cha "Sirah al-Ulama"

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha